Thursday, February 13, 2020

Fonetiki ya Kiswahili

Tofauti ya dhana ya Fonetiki
CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA ZANZIBAR
(SUZA)
SKULI YA KISWAHILI NA LUGHA ZA KIGENI
(SKILUKI)
IDARA YA KISWAHILI

JINA LA KOZI:           NADHARIA YA FONETIKI NA FONOLOJIA YA KISWAHILI
KODI YA KOZI:         LK 2101
MHADHIRI:              MR. AMOUR A. KHAMIS
MWAKA:                    MWAKA WA PILI
MUHULA:                  MUHULA WA KWANZA
KAZI:                          KAZI YA NYUMBANI
WASHIRIKI:              ABDI NASSOR HAJI                           BAE/17/18/125/TZ
                                    MWANAIDI BILAL KASIM                BAE/17/18/132/TZ
                                                        
SUALI:            ‟ Linganisha na tofautisha dhana ya fonetiki iliyotolewa na Khamis na Masamba
TAREHE YA KUWASILISHA: 20/11/2019

Kwa mujibu wa  Khamis  (2011)  "Fonetiki ni tawi la lughawiya fafanuzi linalochunguza taaluma ya uchambuzi na uchanganuzi wa vitamkwa vya lugha mbalimbali zitumiwazo na mwanaadamu katika hali ya utamkwaji, usafirishwaji na usikiwaji pamoja na uandikwaji wa vitamkwa hivyo kifonetiki kutoka uandikwaji wa kiothografia ".
Vilevile Masamba, (2007) kaeleza maana ya fonetiki kuwa “ni tawi ambalo linajisughulisha na uchunguzi na uchanganuzi wa taratibu zote zonazohusiana na utoaji, utamkaji, usafirishaji, usikiaji na ufasili wa sauti za lugha za binaadamu kwa ujumla
Hivyo basi, kutokana na fasili zilitolewa na wataalamu hao hapo juu  kwa ujumla wake tunapata maana kuwa fonetiki ni tawi la lughawiya ambalo dhumuni lake ni kuchunguza na  kuchambua jinsi vitamkwa au sauti za lugha mbali mbali zinavyotamkwa, kusafirishwa ( kupitia mkondo hewa ) na  jinsi zinavyosikika. Katika kuangalia vitamkwa au sauti za lugha, tunaangalia kupitia matawi ya fonetiki ambayo ni fonetiki matamshi, fonetiki akustika na fonetiki masikizi.
Maana hizo hapo juu zinaelekea kulingana kwa ujumla wake pia kutofautiana kwa baadhi ya vipengele kama ifuatavyo:
Kwa upande wa kufanana au kulingana wataalamu hao wamefanana katika kuzungumzia swala la sauti za lugha ya mwanaadamu. Fonetiki hushughulikia sauti za lugha pekee na si sauti nyenginezo zinazotokana na binadamu kama vile kucheka, kulia au hata chafya ambapo sauti hizi haziwezi kuwa ni vitamkwa vya lugha. Hivyo wataalamu hawa walipotoa fasili ya fonetiki wamezingatia suala la msingi ambalo ni sauti za lugha au vitamkwa vya lugha ya mwanaadamu ambavyi kimsingi ndivyo vyenye kushughulikiwa na tawi hili. Wanafonetiki huchunguza jinsi sauti za lugha zinavotamkwa, kusafirishwa Kati ya kimyaa cha msemaji na sikio la msikilizaji na jinsi zinavyofasiriwa katika ubongo wa msikilizaji.
Vilevile, wataalamu wote wawili wamezungumzia tawi la lughawiya. Kimsingi hasa fonetiki ni tawi la lughawiya: ambapo tawi hili hujikit akatiak uchanganuzi wa ndani kabisa wa vitamkwa vya lugha za binnadamu. Katika maana za wataalamu wa hapo juu tunaona kuwa wataalamu hao hawakuacha kuingiza maneno hayo ambayo ni tawi la lughawiya au tawi la isimu, hivyo huwezi kuipata fonetiki kwenye fani yoyote isipokua katika isimu au lughawiya.
Pia, wataalamu wote wametumia neno mwanaadamu. Mwanaadamu ndie kiumbe pekee ambae ana uwezo wa kuzalisha vitamkwa vya lugha ambavyo vinaweza kusikika, kufahamika na kuandikika na pia binadamu pekee ndie mwenye uwezo wa kutumia lugha. Hivyo, wataalamu hawa hawakuacha kulitumia neno hili kwani wanyama hutoa milio tu ambayo inasikika ila haiwezi kufahamika wala kuandikika wala kubainishwa kifonetiki bali ni njia yao ya mawasiliano.
Kwa kuongezea, wataalamu hawa wamezungumzia suala la utamkwaji, usafirishwaji na usikiwaji wa sauti za lugha. Hii ina maana kua Khamis na Massamba wanakubaliana kuwa sauti zote za lugha lazima zitamkike (kutoka katika kinywa cha binaadamu), zisafirishwe ( sauti ziwe ni zenye kubebwa na mkondo hewa ) na kusikika ( msikilizaji awe anazisikia na kuzifahamu ). Katika kutoa fasili zao wamezingatia matawi ya fonetiki ambayo ni fonetiki matamshi (utamkwaji ), fonetiki akustika (usafirishwaji) na fonetiki masikizi (usikiwaji)
Kwa upande mwengine, Khamis na Massamba katika fasili yao ya fonetiki wametofautiana kwenye vipengele vichache kama ifuatavyo:
Massamba kwenye fasili ya dhana fonetiki kaeleza kuwa fonetiki ni taaluma inayojihusisha na utoaji wa sauti za lugha….ikiwa na maana kua fonetiki inahusiana kule tu sauti za lugha kutolewa katika kinywa cha msemaji. Ambapo Khamis kaelezea kua fonetiki inahusiana na uchambuzi na uchanganuzi wa vitamkwa vya lugha ikiwa na maana kuwa Khamis yeye kazingatia uchambuzi na uchanganuzi wa sauti hizo ambazo huzalishwa kutoka katika kinywa cha msemaji.
Kwa ujumla wake licha ya toafati ndogo ndogo zilizojitokeza kwenye fasili za wataalamu hao ila kwa kiasi flani wameweka wazi lile lengo hasa na kazi hasa ya fonetiki kua ni kuchunguza sauti za lugha na si vyenginevyo. Utoafauti huo uliotokea ni kile kinachoitwa upekee wa mtu, hii ni kwa sababu mada moja haiwezi kulezewa sawa sawa na watu wawili tofauti, kila mmoja ataelezea kiupande wake ila lengo na dhumuni huwa ni lilelile.



MAREJEO
Khamis,A. (2011). Uchambuzi wa Kiswahili Fasaha: Sarufi na Lughawiya. Chuo Kikuu cha Elimu Chukwani. Zanzibar.
Massamba, D. (2007).Fonolojia ya Kiswahili Sanifu.Taasisi ya Uchunguzi wa Kiswahili. Dar Es Salaam.
Mgullu, S.R. (1999). Mtaala wa Isimu:Fonetiki , Fonolojia na Mofolojia ya Kkiswahili. Nairobi, Printwell Industries.

No comments:

Post a Comment

Thanks